Posts

TUTAWAFUNGA SIMBA KWA TAHADHARI….HUWA WANAPANIA SANA MECHI HII…

Image
  KOCHA Mkuu wa Yanga , Miguel Gamondi ameonekana bado anahitaji kuwa makini mbele ya Simba kwa kutumia muda wa kutazama michezo yote mikubwa waliocheza wapinzani wao hivi karibuni. Hatua hiyo kuelekea katika mchezo wa Kariakoo Derby dhidi ya Wekundu wa Msimbazi hao kwa kuhitaji msimu huu kuvuna alama zote sita zile za mzunguko wa kwanza walizoshida bao 5-1 na Jumamosi hii kutafuta ushindi. Yanga watakuwa wenyeji ikiwakaribisha Simba mchezo huo utakaochezwa Jumamosi hii katika dimba la Benjamin Mkapa Dar es Salaam, saa 11:00 jioni. Kocha huyo ameamua kukaa na wachezaji kupitia michezo mbalimbali ili kuweza kila mmoja anawezaje kufanya majukumu yake. Kwa mujibu wa Gamondi kuwa licha ya Simba kutokuwa vizuri hivi karibuni lakini mpinzani wake huyo amekuwa hatari hasa katika mechi kubwa na kumlazimi kuanza kufatilia na kuona ubora wao. Amesema ameona uimara wa safu ya ushambuliaji, viungo na ulinzi kwa wapinzani wake ikiwrmo kwenye upigaji wa mipira ya vichwa na kutakiwa kufanyia kazi kil

Watu 26 washambuliwa na mbwa Mwananyamala

Image
Wakazi 26 wa Wilaya ya Kinondoni wakiwemo watoto wameshambuliwa na kujeruhiwa na mbwa anayedaiwa ana kichaa alipokuwa akizurura maeneo ya Mwananyamala. Kati ya waliong'atwa wapo watoto 20 wa kuanzia miaka minne hadi 12 na watu wazima sita, ambao ni wakazi wa mitaa ya Kambangwa, Kinondoni na Mwananyamala kwa Kopa. Akizungumza leo Jumamosi Machi 9,2024 na Mwananchi Digital, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano serikalini Manispaa ya Kinondoni, Aquilinus Shiduki amesema mbwa huyo na wengine wawili tayari wameshauliwa katika msako wa kumtafuta baada ya kufanya tukio hilo. “Ni kweli tukio hilo lilitokea jana kwa watu kushambuliwa na mbwa huyo, lakini baada ya kuripotiwa, msako mkali ulifanyika jana na kufanikiwa kumkamata na kumuua. “Katika msako huo ambao ni endelevu, leo tena tuliwakamata mbwa wengine wawili waliokutwa wakizurura, maofisa wetu wa wanyama wakawaua na kufanya mbwa waliouawa hadi sasa kufika watatu,”amesema Shiduki. Kutokana na tukio hilo, amewatahadharisha watu wenye kufu

Ubovu wa barabara wananchi washindwa kupata mahitaji

Image
  Baadhi ya wanakijiji wa kijiji cha Mnyangara Kata ya Mipingo Manispaa ya Lindi wamekosa huduma ya barabara kwa takribani wiki mbili baada ya mvua kuharibu miundombinu ya Daraja la Mto Mangoma na kushindwa kupitika. Kutokana na changamoto hiyo, leo Machi 9, 2024 baadhi ya wanakijiji wamejitolea kutengeneza njia ya muda ili huduma ya barabara iweze kurejea kijijini hapo. Akizungumza wakati kazi hiyo ikiendelea, mmoja wa wanakijiji amesema kwa wiki mbili wamekosa huduma muhimu kwa kutopitika kwa barabara hiyo. "Kwa wiki mbili hatukuweza kupata huduma za kijamii nje ya kijiji chetu, kutokana na mvua kunyesha, maji yameanzisha mfereji mpya na kusababisha upande mmoja wa daraja kushindwa kupitika,” amesema. “Baaada ya maji kupungua leo tumejitokeza wananchi kuja kutengeneza barabara ya dharura itakayosaidia kupita hata trekta, pikipiki na watembea kwa miguu tu." Mkazi mwingine wa kijijini hapo amesema hofu yao ni kama angetokea mjamzito anayetakiwa kuwahishwa hospitalini. "T

Yanga inabeba tena

Image
Samson Mbangula anaumaliza msimu wa Simba katika Ligi Kuu Bara kirahisi pale Jamhuri, Morogoro. Mabao yake mawili ni kilio kipya Msimbazi kwa kuzima ndoto za kuwania ubingwa msimu huu. Kipigo kizito. Kipigo cha maumivu kwa Wanasimba wote. Ushindi wa Tanzania Prisons mbele ya Simba pale Morogoro ni kama mpasuko mkubwa katika jahazi lililo katikati ya Bahari. Imeziweka hesabu za Simba kuwania ubingwa msimu huu kuwa ngumu kabisa. Simba hata ikishinda mchezo wa kiporo dhidi ya Mtibwa Sugar bado itakuwa imeachwa alama saba na Yanga. Ni alama nyingi mwa Mnyama kuweza kuzifikia. Hesabu ni ngumu sana kwa Simba. Unaweza kuona kuwa alama saba sio nyingi, ila kiwango cha Simba kwenye ligi kinafanya zionekane nyingi sana. Simba hawana uhakika wa kushinda mechi tano mfululizo Simba haina uhakika wa kushinda mechi za dabi dhidi ya Azam FC na Yanga. Hivyo uwezekano wa wigo huo wa alama kuongezeka ni rahisi zaidi kuliko kupungua. Kiwango cha sasa cha Yanga ni vigumu kuzuilika. Yanga ipo kwenye ubora w

Makundi ya Haiti yajaribu kuuteka uwanja wa ndege wa Port-au-Prince

Image
Wanajeshi wamepelekwa ili kulinda uwanja wa ndege wa mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince, dhidi ya kushambuliwa na makundi yenye silaha. Mashahidi waliripoti kusikia milio ya risasi  karibu na Uwanja wa Ndege wa Toussaint Louverture huku vikosi vya usalama vikikabiliana na watu waliokuwa na silaha nzito. Lengo la makundi hayo ni kumzuia Waziri Mkuu Ariel Henry kurejea Haiti, ambaye anaaminika kuwa nje ya nchi. Ghasia zimeongezeka bila kuwepo kwake huku magenge ya watu wakimtaka ajiuzulu. Bw Henry aliondoka Haiti wiki iliyopita ili kuhudhuria mkutano wa kilele wa kikanda huko Guyana. Baada ya hapo, alisafiri hadi Kenya kutia saini mkataba wa kutumwa kwa jeshi la polisi wa kimataifa nchini Haiti. Waziri Mkuu kwa sasa hajulikani aliko lakini msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani alisema: "Tunafahamu kwamba waziri mkuu anarejea nchini [Haiti]". Akiwa nchini Kenya, muungano wa magenge ukiongozwa na afisa wa zamani wa polisi, Jimmy "Barbecue" Chérizier, ulishambuli

Soko la madini lahitajika haraka Tunduru

Image
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro ameagiza kukamilishwa ujenzi wa soko la kisasa la madini ya vito litakalokuwa kubwa zaidi Afrika Mashariki. Soko hilo linajengwa katika Halmashauri ya wilaya hiyo kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kusaidia kukomesha mianya ya utoroshaji wa madini. Agizo hilo amelitoa leo Jumatatu Machi 4, 2024 baada ya kutembelea ujenzi wa soko hilo akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya. Mtatiro amesema amefurahishwa na hatua za ujenzi huo, anaosema una tija kwa mustakabali wa rasilimali za Tanzania. "Naelekeza uongozi wa Halmashauri ya Tunduru kukamilisha haraka ujenzi wa soko hili la kisasa la madini ya vito na lianze kufanya kazi kwa wakati,” amesema mkuu huyo wa wilaya Mtatiro. Amesema likianza litasaidia kupunguza kama si kumaliza vitendo vya utoroshaji wa madini ya vito wilayani humo. Amaesema utoroshaji huo unafanywa na wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wanasababisha Serikali kukosa mapato na kodi. Amefaf

Dondoo za Soka Kimataifa

Image
  Brentford wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Norwich na Marekani Josh Sargent, 24, huku wakijiandaa kwa ajili ya kuondoka kwa mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 27, ambaye anazivutia Chelsea na Arsenal. (Football.London) Manchester City na Borussia Dortmund wanamfuatilia mshambuliaji wa AC Milan wa timu ya taifa ya Italia chini ya umri wa miaka 17 Francesco Camarda, ambaye anatazamiwa kukataa ofa ya mkataba wa kulipwa katika klabu hiyo ya Serie A atakapofikisha umri wa miaka 16 wiki ijayo. (Gazzetta dello Sport via Football Italia) Arsenal wamempa kipaumbele mshambuliaji wa Sporting Lisbon na Uswidi Viktor Gyokeres, 25 msimu huu. (TodoFichajes - kwa Kihispania) Liverpool wanatazamiwa kuanza mazungumzo na Andy Robertson kuhusu kandarasi mpya msimu huu wa joto na hawana wasiwasi na ripoti zinazomhusisha mlinzi huyo wa kushoto wa Scotland mwenye umri wa miaka 29 na Bayern Munich. (Football Insider) Baba yake Khvicha Kvaratskhelia anasema winga huyo wa Georgia mwenye umri wa miaka 2